»Video za uzalishaji kutoka kwa Wadep: Asali«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=W26pfB2aZT8&t=101s

Muda: 

00:05:32
Imetengenezwa ndani: 
2010

Imetayarishwa na: 

IICD.org

Ufugaji wa nyuki ni mojawapo ya fursa za kibiashara zenye faida kubwa miongoni mwa wafugaji, kwani asali ni chanzo cha faida nyingi za kiafya na kimapato.

Kabla ya kuvuna asali mfugaji anatakiwa kuandaa na kupanga vifaa vya kimsingi vinavyohitajika kama vile mavazi, kofia na barakoa, glovu za mikono, gumbooti, ​​ndoo yenye mfuniko, kitoa moshi, kisu na viberiti ili kuhakikisha usalama wakati wa kuvuna.

Shughuli za kabla ya kuvuna

Vaa nguo za kujikinga kila mara na hakikisha kwamba umelindwa vya kutosha. Jaza kitoa moshi na nyenzo za kutosha ambazo zitadumu katika kipindi cha kuvuna.

Washa kitoa moshi na uvae mavazi ya kuvunia asali.

Shughuli za kuvuna

Puliza moshi kuanzia kando mwa mzinga, chini ya mfuniko na mlangoni ili kusababisha nyuki wanaozunguka mlango kurejea ndani ya mzinga.

Kisha ondoa mfuniko na upulize moshi ili kuhakikisha nyuki walioko juu ya mzinga wanaingia ndani. Tambua pande isiyo na asali, na kwa kutumia kisu gonga mbao za juu kwani masega matupu hufanya kelele kubwa zaidi.

Tumia kisu kuondoa mbao za juu ukianzia upande usio na masega. Pulizia moshi kwa nyuki zilizo kwa masega. Ondoa nyuki kwa upole na uwaingize ndani ya mzinga. Kata masega yaliyokomaa na uyaweke ndani ya chombo.

Safisha pande za mbao za juu, zipange tena kama vile zilivyokuwa awali. Pulizia moshi kwenye juu yazo ili kuwafanya nyuki wote kuingia kwenye mzinga.

Usindikaji wa asali

Anza kwa kuvunja masega ukitumia kisu, yaweke kwenye kichungi safi, funika na kitambaa safi juu ya ndoo.

Funika chombo na mfuniko ili hewa isiingie. Hifadhi asali iliyochujwa kwenye vyombo vya plastiki.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:23Uvunaji na usindikaji wa asali.
00:2401:06Vifaa vya kimsingi vinavyohitajika; mavazi, kofia na barakoa, glovu za mikono, gumbooti, ​​ndoo yenye mfuniko, kitoa moshi, kisu na viberiti
01:0701:13Shughuli za kabla ya kuvuna.
01:1401:35Vaa nguo za kujikinga. Jaza kitoa moshi na nyenzo za kutosha.
01:3602:38Washa kitoa moshi na uvae mavazi ya kuvunia asali.
02:3902:45Shughuli za kuvuna.
02:4603:06Puliza moshi kuanzia kando mwa mzinga, chini ya mfuniko na mlangoni
03:0703:25Subiri kwa muda na ufungue vipande vya mbao vilivyo juu ya mzinga kwa upole, piliza moshi juu ya vipande hivyo.
03:2603:48Tambua pande isiyo na asali kwa kutumia kisu. Ondoa mbao za juu ukianzia upande usio na masega.
03:4904:02Pulizia moshi kwa nyuki zilizo kwa masega. ondoa nyuki kwa upole na uwaingize ndani ya mzinga. Kata masega yaliyokomaa na uyaweke ndani ya chombo.
04:0304:12Safisha pande za mbao za juu, zipange tena kama vile zilivyokuwa awali, kisha ulizia moshi juu yazo.
04:1304:31Shughuli za usindikaji wa asali. vifaa; ndoo safi na kichungi.
04:3204:58Vunja masega ukitumia kisu, yaweke kwenye kichungi safi, funika na kitambaa safi juu ya ndoo.
04:5905:10Funika chombo na mfuniko. Hifadhi asali iliyochujwa kwenye vyombo vya plastiki.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *