»Kanuni za uhimilishaji bandia (AI)»

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=KkT79NAw6kc

Muda: 

00:13:46
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Digital Agriculture

Uhimilishaji Bandia (AI) ni mchakato ambao shahawa (mbegu) huwekwa ndani ya mfumo wa uzazi wa mnyama jike ili atunge mimba.

AI husaidia kueneza shahawa kutoka kwa dume aliye na sifa bora na kuzuia kuenea kwa magonjwa yanayonezwa wakati dume akimpanda jike. Kuna vifaa kadhaa vinavyohitajika kama vile mtungi wa kuhifadhia mbegu ambao huwekewa hewa ya nitrojeni, mrija wa shahawa iliyogandishwa, bomba la kukusanya shahawa, mkasi, kipimajoto, maji ya vuguvugu. Hakikisha hakuna pengo kati ya mkato wa mrija wa shahawa na nailoni ili kuzuia sehemu ya shahawa isibaki kwenye mrija. Uke wa mnyama unapaswa kutambuliwa na mtu aliye na ujuzi juu ya uzazi.

Hatua za kufuata

Anza kwa kutambua nambari ya dume kutoka kwa lebo iliyoambatanishwa kwenye mtungi. Kisha inua chombo kilicho ndani ya mtungi hadi kitakapofika shingoni mwa mtungi. Chukua mrija wa shahawa ukitumia kibano kwa haraka iwezekanavyo na uziunde ili kuondoa nitrojeni ya ziada.

Zingatia hali joto sahihi na wakati unapoweka mrija wa shahawa kwenye maji ya joto ili kufikia kiwango cha juu cha uponaji wa shahawa.

Baada ya kuyeyusha, futa mrija wa shahawa kwa upole ili kuondoa maji.

Kisha weka karatasi ya nailoni juu ya kifaa cha kuingiza shahawa na uimarishe na pete. Hakikisha umevaa glavu za kujikinga ili kuepuka maambukizi, tumia vilainishi na upanue vizuri mfumo wa uzazi.

Fungua mlango wa uke na ingiza kifaa cha kuingiza shahawa kwa pembe ya 30– 40 ili kuepuka ufunguzi wa tundu la mkojo. Chomeka kifaa cha kuingiza shahawa kwa upole hadi kitakapofika kwenye kuta za ndani za tumbo la uzazi.

Baada ya kutenda mchakato wa AI, kanda kwa upole kisimi mara kumi ili kupata matokeo mazuri. Mwisho, uhimilishaji bandia unafaa kufanywa katika nyakati zinazofaa ili kupata kiwango cha juu cha utungaji mimba.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:48AI husaidia kueneza shahawa kutoka kwa dume aliye na sifa bora na kuzuia kuenea kwa magonjwa yanayonezwa wakati dume akimpanda jike.
00:4903:10Vifaa kadhaa vinavyohitajika:mtungi wa nitrojeni, mrija wa shahawa iliyogandishwa, bomba la kukusanya shahawa, mkasi, kipimajoto, maji ya vuguvugu.
03:1103:56Tambua nambari ya dume, inua chombo kilicho ndani ya mtungi hadi kitakapofika shingoni mwa mtungi na uchukue mrija wa shahawa.
03:5705:27Chukua mrija wa shahawa ukitumia kibano kwa haraka iwezekanavyo na uziunde.
05:2806:49Zingatia hali joto sahihi na wakati unapoweka mrija wa shahawa kwenye maji ya joto.
06:5007:16Baada ya kuyeyusha, futa mrija wa shahawa kwa upole ili kuondoa maji.
07:1707:44Weka mrija wa shahawa kifaa cha kuingiz shahawa na uukate ifaavyo.
07:4508:09Kisha weka karatasi ya nailoni juu ya kifaa cha kuingiza shahawa na uimarishe na pete.
08:1008:35Hakikisha hakuna pengo kati ya mkato wa mrija wa shahawa na nailoni
08:3609:32Hakikisha umevaa glavu za kujikinga,kisha tumia vilainishi na upanue vizuri mfumo wa uzazi.
09:3310:43Fungua mlango wa uke na ingiza kifaa cha kuingiza shahawa
10:4411:28Chomeka kifaa cha kuingiza shahawa kwa upole hadi kitakapofika kwenye kuta za ndani za tumbo la uzazi.
11:2911:56Kifaa cha kuingiza shahawa kinapofika kwenye kuta za ndani ya tumbo la uzazi, weka shahawa ndani kwa upole.
11:5712:48Baada ya kutenda mchakato wa AI, kanda kwa upole kisimi mara kumi ili kupata matokeo mazuri.
12:4913:08Kamasi kutoka kwa uke ni dalili nzuri ya wakati ufaoo kutekeleza uhimilishaji bandia.
13:0913:46Tekeleza uhimilishaji bandia siku hiyo hiyo ukiona dalili hizo.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *