»jinsi ya kukuza vitunguu«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=7yw_R6wPi-k

Muda: 

00:20:13
Imetengenezwa ndani: 
2021

Imetayarishwa na: 

FARM MATTERS

Uanzishaji na usimamizi sahihi wa kitalu ni muhimu ili kuhakikisha uotaji bora wa mbegu.

Baada ya kupanda, mbegu huchukua siku 5 hadi 10 kuota. Iwapo asilimia 50 ya mbegu zimeota, ondoa matandazo kwenye kitalu na mwagilia maji. Uondoaji wa matandazo katika hatua hii huzuia uingiaji wa miche kwenye matandazo, jambo ambalo husababisha uharibifu wa miche wakati wa kuondoa matandazo.

Usimamizi wa kitalu

Siku moja hadi mbili baada ya kuondoa matandazo, nyunyizia viuakuvu kwenye miche ili kuzuia ukungu, na kisha endelea kunyunyizia dawa mara kwa mara baada ya muda maalum.

Siku nne baada ya kuondoa matandazo, weka mbolea ya majani, huku ukiongeza dawa ya kuua wadudu baada ya siku 5 hadi 7.

Wakati miche ina umri wa wiki 4, badilisha mbolea ya majani na uweke mbolea ambayo husaidia miche kustawi na kuwa migumu kwa ajili ya kupandikizwa.

Daima dhibiti magugu. Inashauriwa kutumia mikono kupalilia ili kutoathiri mizizi. Pia hakikisha kwamba sehemu ya juu ya kitalu imesawazishwa ili kuzuia mmomonyoko wa udongo.

Kupandikiza

Iwapo miche iko tayari kupandikizwa, lakini hakuna mvua wa kutosha, itolee miche virutubisho vidogo ili kupunguza kuaji.

Ikiwa ardhi yako ina mwinuko, tengeneza matuta bila kufwata mteremko ili kudhibiti mmomonyoko wa udongo.

Baada ya kupandikiza, dhibiti kwa makini magonjwa na wadudu waharibifu kama vile vidukari, chawa na utitiri.

Ikiwa udongo una fosforasi kidogo, ongeza Di ammoniamu phosphate wakati wa kupandikiza.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0002:45Baada ya kupanda, mbegu huchukua siku 5 hadi 10 kuota.
02:4604:50Iwapo asilimia 50 ya mbegu zimeota, ondoa matandazo
04:5105:56Siku moja hadi mbili baada ya kuondoa matandazo, nyunyizia viuakuvu
05:5706:25Siku nne baada ya kuondoa matandazo, weka mbolea ya majani
06:2606:45Nyunyiza dawa ya kuua wadudu baada ya siku 5 hadi 7.
06:4607:25Wakati miche ina umri wa wiki 4, badilisha mbolea ya majani na uweke mbolea ambayo husaidia miche kustawi.
07:2607:52Daima dhibiti magugu
07:5311:06Hakikisha kwamba sehemu ya juu ya kitalu imesawazishwa ili kuzuia mmomonyoko wa udongo.
11:0714:13Tolea miche virutubisho kidogo ili kupunguza kuaji iwapo kupandikiza kutacheleweshwa.
14:1417:45Kwa ardhi iliyo na mwinuko, tengeneza matuta bila kufwata mteremko ili kudhibiti mmomonyoko wa udongo.
17:4620:06Baada ya kupandikiza, dhibiti kwa makini magonjwa na wadudu waharibifu kama vile vidukari, chawa na utitiri.
20:0720:13Ikiwa udongo una fosforasi kidogo, ongeza Di ammoniamu phosphate.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *