»Jinsi ya kupanda maharagwe«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=7PvezpWIkdA

Muda: 

00:14:44
Imetengenezwa ndani: 
2021

Imetayarishwa na: 

Best Farming Tips

Maharagwe huongeza nitrojeni kwenye udongo na yana protini nyingi. Ukuaji wao unahitaji hatua chache, kwani maharagwe hupandwa moja kwa moja shambani.

Maharagwe huhitaji jua la kutosha, na udongo wenye unyevu na rutuba kwa ukuaji sahihi. Inashauriwa kuboresha pH ya udongo hadi 5.5–5.8 kwa kuongeza chokaa, kwani maharagwe huathiriwa na tindikali. Joto la udongo linapaswa kuwa 60–70 F kwa ukuaji sahihi. Acha umbali wa cm 10–15 kati ya mimea ni umbali wa 45cm kati ya safu. Loweka mbegu kwa saa 24 kabla ya kupanda ili kusaidia kuhimiza uotaji.

Hatua zinazozingatiwa

Anza kwa kuandaa shamba mapema, jaza mashimo na samadi iliyooza kwa ukuaji bora wa mmea.

Pia tengeneza mtaro wa mboji wenye kina cha sentimita 30 ambapo maharagwe yatapandwa na uujaze samadi ya wanyama ili kuongeza ukuaji. Panda mbegu safi, na ongeza viwango vya mbolea vilivyopendekezwa.

Maharage yanapofika mwezi 1, weka kilo 50 ya mbolea ya jasi kwa ekari ili kusaidia kutoa maganda, na naitrojeni.

Kisha chimba mashimo ya kupandia kwa kina cha cm 2.5–5, na panda mbegu 2–3 kwa kila shimo. Mwagilia mimea asubuhi ili kuzuia mnyauko na kudhibiti magonjwa ya ukungu. Acha umwagiliaji wakati asilimia 25% ya maganda ya maharagwe yamegeuka manjano.

Pia panda maharagwe pamoja na mahindi ili kulinda maua ya maharagwe wakati wa mvua. Katika hatua ya kuchanua maua, weka mbolea ya jasi kwa kiwango cha kilo 200 kwa kila hekta au samadi ya wanyama ili kuongeza mavuno.

Kila mara palilia shamba kwa mkono ili kuepuka kuharibu mizizi ya mimea, na kuvuna kwa wakati ufaao kulingana na aina ya maharagwe.

Pia weka mwarobaini au shaba kwa wakati ufaao ili kuzuia magonjwa ya ukungu, na fanya mzunguko wa mazao ili kudhibiti magonjwa yanayoenezwa na mizizi. Epuka kufanya kazi shambani wakati majani yana unyevu ili kuzuia kueneza magonjwa ya ukungu na bakteria.

Mwishowe, kagua shamba kila mara ili kuangalia milipuko ya magonjwa.

Aina za maharagwe

Maharage ya kichaka; haya ni mafupi, hukua hadi urefu wa 60cm na hayahitaji vijiti vya kuhimili mmea.

Maharagwe aina ya pow, haya hukua hadi kufikia urefu wa mita 2.4– 3, huhitaji vijiti vya kuhimili mmea, ni rahisi kuvunwa na hutoa mavuno mengi. Aina zingine za maharagwe ni pamoja na maharagwe ya runners, maharagwe ya lima, mbaazi na maharagwe ya soya.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:03Maharagwe huongeza nitrojeni kwenye udongo na yana protini nyingi.
01:0401:25Lowekwa mbegu kwa saa 24 kabla ya kupanda.
01:2602:47Aina za maharagwe
02:4803:43Hatua za kufuata unapopanda maharagwe
03:4404:01Maharagwe huhitaji jua la kutosha, na udongo wenye unyevu na rutuba
04:0205:08Tengeneza mtaro wa mboji wenye kina cha sentimita 30 ambapo maharagwe yatapandwa na uujaze na samadi ya wanyama
05:0905:38Panda mbegu safi. Unapotumia mbolea za madini, ziweke ipaswavyo na zichanganye vizuri na udongo.
05:3906:13Maharage yanapofika mwezi 1, weka kilo 50 ya mbolea ya jasi, na naitrojeni.
06:1406:50Boresha pH ya udongo hadi 5.5–5.8. Joto la udongo linapaswa kuwa 60–70 F.
06:5107:50Acha umbali wa cm 10–15 kati ya mimea ni umbali wa 45cm kati ya safu.
07:5108:13Chimba mashimo ya kupandia kwa kina cha cm 2.5–5, na panda mbegu 2–3 kwa kila shimo.
08:1409:37Weka vijiti vya kuhimili mmea kabla ya kupanda. Mwagilia mimea asubuhi.
09:3810:03Panda maharagwe pamoja na mahindi . Acha umwagiliaji wakati asilimia 25% ya maganda ya maharagwe yamegeuka manjano.
10:0410:32Katika hatua ya kuchanua maua, weka mbolea ya jasi kwa kiwango cha kilo 200 kwa kila hekta au samadi ya wanyama
10:3311:44Mwagilia mimea mara 2- 3 kwa wiki. ng‘oa magugu. Vuna maharagwe katika wakati sahihi. Hifadhi maharagwe vizuri.
11:4512:10Magonjwa na wadudu ya maharagwe
12:1113:21Weka mwarobaini au shaba kwa wakati ufaao. Epuka kufanya kazi shambani wakati majani yana unyevu
13:2214:44Weka dawa za kemikali zilizopendekezwa. Kagua shamba kila mara

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *