Jinsi ya kupandikiza miche – mwongozo

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=5tOwc3VCuTo

Muda: 

00:02:34
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

FarmKenya
Kupandikiza ni mchakato wa kuhamisha mmea kutoka sehemu moja hadi nyingine, na kutunza miche katika mazingira salama.
Kupandikiza ni mchakato nyeti lakini hutoa faida nyingi kwa wakulima. Kutumia miche ni njia rahisi na ya kawaida ya kuanzisha kilimo cha mboga. Miche ni mbegu zilizoota.

Masharti

Wakati ufaao wa kupandikiza miche hutegemea ukuaji wa majani ya kweli yaliyotofauti na majani ya mapema. Kabla ya kupandikiza hakikisha udongo una ubora mzuri, na uwezo wa kushika unyevu.
Pandikiza miche alasiri ili kusaidia mmea kupona wakati wa kupandikiza.

Kuimarisha miche

Hapa ndipo unapoanza kuzoeza miche mazingira yao ya baadaye na ya kudumu. Ni hatua muhimu kwa mafanikio ya mmea.
Miche huhitaji muda ili kuzoea mazingira mapya kabla ya kupandikizwa. Kwa muda wa wiki moja hadi mbili, acha miche izoee mazingira mapya.

Kupandikiza

Tumia jembe, sepeto au mwiko kutengeneza shimo dogo shambani. Tengeneza mashimo kwa kina kulingana na mizizi ya mmea. Hakikisha kwamba mizizi imeshikiliana na udongo.
Weka mmea ndani ya shimo na ujaze nafasi iliyobaki na udongo wenye rutuba. Nyunyizia maji kwenye udongo uliozunguka mmea ili kuruhusu mizizi kufikia virutubisho.

Mshtuko wa kupandikiza

Ikiwa mmea utaanza kunyauka, au kugeuka na kuwa rangi ya manjano kutokana na jua kali, tolea mimea kivuli.
Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:35Jinsi ya kupandikiza miche.
00:3601:06Kuimarisha miche
01:0702:07Kupandikiza
02:0802:24Mshtuko wa kupandikiza mimea.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *