»Kukuza mananasi«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=Y8Hly2qFyqk

Muda: 

00:11:23
Imetengenezwa ndani: 
2022

Imetayarishwa na: 

AGRIMAT USA

Mananasi yanahitajika sana, na yanapendekeza halijoto la nyuzi joto 21 – 29 Celsius na mvua wa wa wasitani wa takribani 600mm. Kujifunza mapendekezo yao ya ukuaji husaidia kuongeza uzalishaji.

Panda kwenye mteremko tambarare kwa ajili ya kuondoa maji ya ziada shambani. Fanya kilimo cha mzunguko wa mazao. Pumzisha na usilime shamba kwa miaka 3. Haya husaidia kudhibiti magugu, wadudu na magonjwa. Uzito wa mbegu (chipukizi) unaokubalika ni kati ya 250 – 450 gramu.

Mapendekezo ya ukuaji

Chagua eneo lililo karibu na barabara kwa usafirishaji rahisi wa pembejeo na mazao hadi sokoni. Pia shamba la mananasi lazima liwe karibu na chanzo cha maji cha kudumu kwani maji ni muhimu kwa shughuli za shamba. Tayarisha ardhi kwa kufyeka, kuchoma na uondoe mashina na mizizi ya miti ili kutunza rutuba ya udongo. Lima shamba mara 2 baada ya muda wa wiki 3 huku ukichanganya udongo mara 2 ili kuruhusu uozo. Tengeneza mitaro yenye upana wa sm 60– 70, urefu wa sm 30 na muachano wa 50 – 60 kati yao ili kudhibiti magugu. Sawazisha uso wa mitaro ili kuzuia mkusanyiko wa maji ambayo yanaweza kusababisha magonjwa ukungu.

Kuweka mbolea

Weka mbolea za mono ammoniamu, salfa ya amonia na urea kwenye mtaro ili kuimarisha rutuba ya udongo. Funika matuta kwa matandazo ya plastiki nyeusi ili kuhifadhi unyevu na kudhibiti magugu. Gueuza mbegu ili sehemu ya chini iangalie juu, kisha weke mbegu juu ya mimea mama na ili mbegu zipate mwanga wa jua. Kata na upunguze baadhi ya sehemu za mbegu. Ondoa mbegu zilizo na magonjwa, na majani ya chini ili kuhimiza ukuzaji wa mizizi na pia kudhihirisha wadudu wanaojificha kama vile matekenya na mchwa. Kabla ya kupanda tibu mbegu kwa dawa iliyopendekezwa. Mwishowe panda kwa sentimita 30 kati ya safu na cm 25 kati ya mimea kwa ukuaji mzuri wa mizizi.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:48Mbinu za kilimo kwa ukuaji sahihi wa mananasi
00:4901:15Mananasi yanahitaji baridi la usiku na mchana la nyuzi joto 21 – 29 Celsius.
01:1602:18Chagua eneo lililo karibu na barabara, lenye udongo usio na maji mengi, lililo karibu na maji ya kudumu.
02:1902:53Kata nyasi, choma na ondoa mashina na mizizi ya miti.
02:5403:55Chagua eneo lisilofurika, panda kwenye mteremko tambarare.
03:5604:13Lima shamba mara baada ya kuvuna
04:1404:42Badilisha mazao, acha shamba bila kulimwa kwa muda wa miaka 3 na upande mazao mapya.
04:4305:05Lima shamba mara 2 baada ya muda wa wiki 3 na ulainishe mara 2.
05:0606:13Tengeneza mitaro yenye upana wa sm 60– 70, urefu wa sm 30 na muachano wa 50 – 60 kati yao. Sawazisha uso wa mitaro
06:1407:17Weka mbolea za mono ammoniamu, salfa ya amonia na urea
07:1807:51Funika mitaro kwa matandazo ya plastiki nyeusi
07:5208:18Chagua nyenzo za upandaji zenye afya, zisizo na magonjwa na zilizoidhinishwa.
08:1908:31Gueuza mbegu na uziweke juu ya mmea mama
08:3208:57Chagua na uchambue mbegu kulingana na uzito na saizi. Punguza uso mkubwa.
08:5809:21Ondoa mbegu zilizo na magonjwa, kasoro, na pia ondoa majani ya chini.
09:2210:34Tibu mbegu kwa dawa inayopendekezwa na kisha vikaushe kwa masaa 2.
10:3511:23Panda kwenye mitarao kwa sentimita 30 kati ya safu na sentimita 25 kati ya mimea.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *