»Kupanda mihogo katika ardhi iliyoinama«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/growing-cassava-sloping-land

Muda: 

00:15:00
Imetengenezwa ndani: 
2017

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Mihogo ni chanzo cha chakula, hata hivyo maji ya mvua husomba udongo wenye rutuba na mavuno ya muhogo hupunguka. Mavuno mazuri ya muhogo yanahitaji kupunguza mmomonyoko wa udongo, na kutunza ardhi yenye afya.

Kwanza, panga mabaki ya mimea kwa muachano ya sentimita 20 kwa mistari ya upinde (contour lines). Panda safu ya nyasi, na jamii ya kunde ili kupunguza mtiririko wa maji ya mvua. Hii husaidia maji kupenyeza na kuacha udongo na virutubisho vilivyosombwa. Pia chimba miinuko au matuta kwenye maeneo yasiyo na bonde sana ili kuboresha jinsi maji yanavyopenyeza ardhini. Weka mbolea ya kikaboni ili kuboresha uzalishaji na rutuba ya udongo. Chimba mashimo ya kupanda ukifata contour kwa muachano wa mita 1. Nafasi hiyo inaweza kupunguzwa ikiwa udongo ni duni sana.

Nitrojeni, Fosforasi na Potasiamu

Unaweza kuongeza virutubisho kwa kutumia samadi au mbolea chache kwa ukuaji bora wa muhogo. Lakini usiweke samadi mbichi juu ya udongo, kwani inaweza kuyeyuka na kusombwa na maji kwa urahisi. Tumia pia N, P, K katika kila shimo la kupanda, kando ya samadi ili kuongeza mavuno. Katakata mashina ya aina bora za mihogo ambazo hutoa majani mengi, kwa urefu wa cm 15 – 20. Weka kila shina katika shimo huku sehemu za macho zikiangalia juu, na sehemu za chini zikiwa kwenye samadi.

Kilimo mseto

Wakati wa miezi 2–3 baada ya kupanda, weka nitrojeni au potasiamu kwani ndivyo virutubisho muhimu kwa muhogo unaokua. Walakini, usiweke mbolea ya madini wakati wa mvua na hali ya kiangazi kirefu ili kuepuka upotezaji wa virutubisho. Panda mimea inayokua kwa haraka ndani ya mihogo ili kulinda udongo dhidi ya magugu, kuongeza kiwango cha nitrojeni kwenye udongo, na kupunguza kazi ya kupalilia. Hakikisha kwamba unajadiliana na wakulima wengine juu ya hatua za kuboresha rutuba ya udongo.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:58Usimamizi sahihi wa udongo huongeza mavuno ya muhogo.
01:5902:10Kupunguza mmomonyoko wa udongo na kujenga mchanga wenye afya.
02:1102:58Panga mabaki ya mimea kwa mistari ya upinde (contour line). Panda safu ya nyasi, na jamii ya kunde.
02:5904:26Pia chimba miinuko au matuta kwenye maeneo yasiyo na bonde sana. Ongeza mbolea ya kikaboni.
04:2705:18Chimba mashimo ya kupandia ukifata mistari ya upinde (contour lines) kwa muachano wa mita 1. Weka mbolea chache katika kila shimo.
05:1905:56Usiweke samadi mbichi juu ya udongo. Tumia N, P, K katika kila shimo la kupanda.
05:5706:34Use high yielding cassava varieties, chop cutting and place with buds facing up.Tumia aina ya mihogo ambayo hutoa mavuno mengi. Kata kata mashina na uyaweke katika shimo huku sehemu za macho zikiangalia juu.
06:3507:13Wakati wa miezi 2–3 baada ya kupanda, weka nitrojeni au potasiamu
07:1408:53Muhogo huhitaji hasa nitrojeni na potasiamu
08:5410:06Weka matandazo kati ya safu za muhogo. Punguza athari za mvua.
10:0712:10Panda mseto wa mihogo na mikunde ya muda mfupi.
12:1112:46Jadiliana na wakulima wengine juu ya hatua za kuboresha rutuba ya udongo.
12:4715:00Muhtasari.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *