»Kutumia safu za nyasi kudhibiti mmomonyoko wa udongo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/grass-strips-against-soil-erosion

Muda: 

00:12:20
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Mmomonyoko wa udongo huwa mwingi katika maeneo yenye mteremko. Mistari ya nyasi iliyopandwa kando ya mtaro (contour) hupunguza kasi ya maji yanayotiririka , na kuruhusu maji yapenyeze kwa udongo na hivyo, kusaidia kudhibiti mmomonyoko. Na pai, hushikilia udongo na viritubisho vilivyo kuwa vimesombwa kutoka juu.

Aina tofauti za nyasi zinaweza kutumika, lakini chagua aina ya nyasi isiyoshindana sana na mazao au kuzaa mbegu nyingi. Unaweza pia kuacha majani ya asili.

Uanzishaji wa nyasi

Mistari ya nyasi inaweza kuanzishwa kwa kutumia mbegu au kung’oa mabonge ya nyasi iliyokomaa. Katika safu moja, panda mistari 3 ya nyasi na kuacha nafasi ya takribani sentimita 20. Unapotumia nyasi zilizong‘olewa, kata nyasi hizo hadi 20cm na ugawanye mashina na mbegu hizo kabla ya kuzipanda. Tumia A frame kupima muinuko wa ardhi au mstari wa contour. Basi panda nyasi katika mashimo ya kina cha sentimita 10cm, acha nafasi ya sentimita 10–20 cm katikati , kisha panda mstari wa pili kando na ule wa kwanza huku ukihakikisha kwamba mashimo yanapitana. Acha nafasi ya mita 20 katika safu za nfasi zilizo kwenye mteremko mpole, na mita 10 kwenye mteremko mkali. Hakikisha kwamba hakutakuwa myanya kwenye safu za nyasi, kwa hivyo lazima zijazwe mwanzoni mwa msimu wa mvua. Nyasi zinaweza kuvunwa kuwa chakula cha mifugo, na kutumika kuandaa chakula cha kuhifadhia mifugo (silage), na kulisha samaki.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:10Mmomonyoko wa udongo huwa mwingi katika maeneo yenye mteremko, na unahitahi usimamizi.
01:1101:59Mistari ya nyasi iliyopandwa kando ya mtaro (contour) hupunguza mmomonyoko wa udongo.
02:0002:14Na pia kuruhusu maji yapenyeze kwa udongo na hushikilia viritubisho vilivyo kuwa vimesombwa kutoka juu.
02:1502:22Aina tofauti za nyasi zinaweza kutumika.
02:2302:37Chagua aina ya nyasi isiyoshindana sana na mazao au kuzaa mbegu nyingi
02:3803:17Unaweza pia kuacha safu nyasi za asili
03:1804:14Tufanya matuta husaidia uoingo kuwa laini, na rahisi kulima.
04:1504:26Mchakato wa uanzishaji wa nyasi
04:2704:31Tumia mbegu au kung’oa mabonge ya nyasi iliyokomaa.
04:3204:44Panda mistari 3 ya nyasi na kuacha nafasi ya takribani sentimita 20
04:4504:51Ukitumia nyasi zilizokomaa, basi kata nyasi hizo hadi 20cm
04:5205:07Gawanye mashina na matawi (mbegu) hizo kabla ya kuzipanda.
05:0805:39Tumia A frame kupima muinuko wa ardhi au mstari wa contour.
05:4005:57Panda nyasi katika mashimo ya kina cha sentimita 10cm, acha nafasi ya sentimita 10–20 cm kati ya mistari.
05:5806:12Panda mstari wa pili kando na ule wa kwanza.
06:1306:26Acha nafasi ya mita 20 katika safu za nfasi zilizo kwenye mteremko mpole, na mita 10 kwenye mteremko mkali.
06:2708:06Nyasi zinaweza kuvunwa kuwa chakula cha mifugo, na kutumika kuandaa chakula cha kuhifadhia mifugo (silage), na kulisha samaki.
08:0708:35Hakikisha kwamba hakutakuwa myanya kwenye safu za nyasi, kwa hivyo lazima zijazwe mwanzoni mwa msimu wa mvua.
08:3610:09Shirikisha wakulima wengine kwa mradi wa kupanda safu za nyasi
10:1012:20Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *