»Mpunga unaopandwa moja kwa moja katika maeneo makavu«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/direct-seeded-rice-dry-conditions

Muda: 

00:08:30
Imetengenezwa ndani: 
2017

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight, Countrywise Communication, Digital Green, IRRI, NARC, Shushilan

Kwa kupanda mbegu za mpunga moja kwa moja kwenye mistari, unaweza kutatua shida ya ukosaji wa maji wakati wa kupiga vidimbwi. Hii hufanyika katika vidimbwi na maeneo makavu pia.

Wakulima wengi hulima mara chache kabla ya kupiga vidimbwi, ambavyo huhitaji mvua nyingi. Kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa, mvua huchelewa kunyesha na hivyo hakuna maji ya kutosha wakati wa kupiga vidimbwi. Hii husababisha mimea kuchelewa kukua, haswa katika shamba lenye mchanga mwepesi.

Kupanda mbegu za mpunga moja kwa moja

Chukua mbegu bora ili kupata mavuno mazuri. Unapotumia dawa za kuua magugu zisizochagua magugu kwa utaratibu, unaweza kudhibiti magugu ambayo yangeweza kuwa shida, haswa katika mwaka wa kwanza. Tumia madawa haya masaa matatu kabla ya kupanda, laa sivyo, utaua mbegu.

Panda mbegu kwenye mistari. Kwa hivyo, unaweza kutumia „lithao“ au zana ya kupanda inayounganishwa na zana ya kulima. Lithao ni kifaa ambacho hutumika kwa mikono. Zana hii hulima mitaro mitatu. Baada ya kutumia lithao, panda mbegu kwa mkono. Kwa kutumia kifaa hiki unahitaji udongo uliyolimwa vizuri, wepesi.

Zana ya kupanda mbegu inayounganishwa na zana ya kulima/mkombo hufanya kila kitu kwa hatua moja. Zana hii hufanya mitaro sita, hupanda mbegu na pia kuifunika kwa mchanga. Kifaa hiki ni nzuri kuokoa wakati na kupanda eneo kubwa.

Manufaa

Zao ambalo limepandwa kwa mbegu moja kwa moja huhitaji maji kidogo, kazi kidogo na pesa kidogo kuliko lile linalopandikizwa. Pia, mavuno yako yatakuwa tayari mapema kwa wiki 1-2.

Kwa kuvuna mapema, unaweza kupanda mazao yanayofuata mapema pia. Mazao ambayo unaweza kupanda wiki moja au mbili mapema ni: viazi, maharadali, ngano au mahindi ya msimu wa baridi. Unaweza hata kupanda zao la tatu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:33Utangulizi
00:3400:44Wakulima wengi hulima mara chache kabla ya kupiga vidimbwi, ambavyo huhitaji mvua nyingi.
00:4500:53Kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa, mvua huchelewa kunyesha na hivyo hakuna maji ya kutosha wakati wa kupiga vidimbwi
00:5401:09Hii husababisha mimea kuchelewa kukua, haswa katika shamba lenye mchanga mwepesi.
01:1001:47Panda mbegu kwenye mistari.
01:4802:04Lithao ni kifaa ambacho hutumika kwa mikono
02:0502:34Zana ya kupanda mbegu inayounganishwa na zana ya kulima/mkombo hufanya kila kitu kwa hatua moja
02:3502:49Zao ambalo limepandwa kwa mbegu moja kwa moja huhitaji maji kidogo, kazi kidogo na pesa kidogo kuliko lile linalopandikizwa.
02:5003:15Mavuno yako yatakuwa tayari mapema kwa wiki moja hadi mbili.
03:1604:35Kwa kuvuna mapema, unaweza kupanda mazao yanayofuata mapema pia
04:3605:50Unapotumia dawa za kuua magugu zisizochagua magugu kwa utaratibu, unaweza kudhibiti magugu ambayo yangeweza kuwa shida, haswa katika mwaka wa kwanza.
05:5106:58Tumia mbegu bora
06:5908:13Muhtasari
08:1408:30Credits

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *