»Teknolojia ya uzalishaji wa mtama baada ya mvua«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=TWOzWUxo69c

Muda: 

00:06:51
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

ICAR-IIMR Millets

Wingi na ubora wa mtama huamuliwa na ubora wa mbegu na mbinu ya uzalishaji.

Mtama ni zao la tano muhimu katika nchi zinazoendelea, na hukuzwa katika maeneo kame, yalio na mvua kidogo, na ukame. Mtama hukuzwa katika msimu wa mvua na baada ya mvua. Ni chanzo cha chakula kwa wanyama katika mfumo wa kilimo cha mchanganyiko wa mazao na mifugo.

Uzalishaji wa mtama

Mtama hustawi katika unyevu uliosalia kwenye udongo, na una tija wa mara 7 kwa hekta. Hii hufanywa kwa kuchagua udongo unaofaa baada ya kuvuna kunde. Tayarisha ardhi kwa kutengeneza mitaro ili kuhifadhi unyevu wa kutosha wakati wa msimu wa upandaji.

Pili, tibu mbegu kwa kutumia kemikali ili kuzilinda dhidi ya shambulio la wadudu na magonjwa. Panda kilo 10 ya mbegu kwa kila hektar. Tengeneza mitaro na weka mbolea huku ukiacha umbali wa sentimita 45×15 kati mimea.

Weka mbolea; kilo 40 ya nitrojeni, na kilo 20 ya fosforasi wakati wa kupanda, na nyunyiza dawa ya kuua magugu baada ya kupanda. Dhibiti magugu na wadudu kwa kunyunyizia dawa siku 25–30 baada ya kupanda. Mtama hukomaa kati ya siku 110–120, hata hivyo huvunwa siku 15 kabla ya siku za kawaida za kuvunia.

Faida za mtama

Mtama hutumika kama chakula kikuu, huku unga wake hutumika kutengeneza chapati, uji, mikate, na malisho ya mifugo. Pia hutumika katika mfumo wa kilimo cha mazao na mifugo ambapo mitama yote huvunwa na mabua huhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye.

Hatimaye, hutumika pia kama chakula, malisho, fumuele, na mazao la madhumuni mbalimbali.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:15Mtama hukuzwa katika maeneo kame, yalio na mvua kidogo, na ukame.
00:1600:20Mtama hukuzwa katika msimu wa mvua na baada ya mvua.
00:2100:42Mtama ni zao la tano muhimu katika nchi zinazoendelea
00:4300:51Ni chanzo cha chakula kwa wanyama katika mfumo wa kilimo cha mchanganyiko wa mazao na mifugo.
00:5201:29Mtama hustawi katika unyevu uliosalia kwenye udongo
01:3001:34Chagua udongo unaofaa baada ya kuvuna kunde
01:3501:44Tayarisha ardhi kwa kutengeneza mitaro ili kuhifadhi unyevu wakati wa msimu wa upandaji.
01:4502:11Aina za mtama ni, phuleyeshoda, parbanimoti na CSH15R.
02:1202:50Tibu mbegu kabla ya kuzipanda.
02:5103:16Tengeneza mitaro na weka mbolea
03:1703:29Panda kwa umbali wa sentimita 45x15 kati mimea. Weka mbolea.
03:3004:08Nyunyiza dawa ya kuua magugu na wadudu baada ya kupanda.
04:0904:31Mtama hukomaa kati ya siku 110–120, hata hivyo huvunwa siku 15 kabla ya siku za kawaida za kuvunia.
04:3204:43Mtama hutumika kama chakula kikuu, huku unga wake hutumika kutengeneza chapati.
04:4405:09Hutumika kutengeneza uji, mikate, na malisho ya mifugo
05:1005:24Pia hutumika katika mfumo wa kilimo cha mazao na mifugo
05:2506:29Mabua ya mtama huhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye au kama malisho ya mifugo.
06:3006:44Mtama hutumika pia kama chakula, malisho, fumuele, na mazao la madhumuni mbalimbali.
06:4506:51Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *