»Uzalishaji wa malisho (nyasi) katika Jamii huko Mandera«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=W0blRPPn3hg

Muda: 

00:08:48
Imetengenezwa ndani: 
2013

Imetayarishwa na: 

Food and Agriculture Organization of the United Nations

Wakati wa ukame au kiangaazi, nyasi ni tatizo kubwa linalowakabili wafugaji katika kulisha mifugo yao, na hii hupunguza ubora wa bidhaa za mifugo.

Ujumuishaji wa mbinu kadhaa za ufugaji hufanywa ili kupunguza changamoto zinazokabiliwa na wafugaji. Jamii hujihusisha na mbinu shirikishi kama vile mbinu bora za ufugaji ili kuzalisha malisho (nyasi) ya mifugo.

Ukuzaji wa nyasi

Chagua eneo la ardhi kwa ajili ya kupanda malisho na uandae ardhi vizuri. Wakati wa kuandaa ardhi, kata miti midogo ili uweze kulima udongo kwa urahisi. Lima ardhi, tengeneza mashimo madogo na chimba mifereji ya kutiririsha maji.

Vile vile baada ya hapo, panda mbegu za nyasi (malisho), Weka maji kwenye mifereji na palilia baada ya siku 14. Baada ya siku 21, ongeza maji shambani mara 3 au 4. Vuna nyasi baada ya siku 45 na uzikaushe kwa siku moja au 2 na kisha uzihifadhi kwa mafungu.

Mbinu za kuhifadhi nyasi husaidia kutoa chakula cha mifugo wakati kinapohitajika, na pia huongeza uwezo wa kustahimili ukame.

Kupitia uzalishaji wa nyasi, jamii hukidhi mahitaji yao na pia huongeza kwenye mlo wao kwa lishe bora. Hii huboresha ustawi wa wakulima.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:01Ujumuishaji wa mbinu kadhaa za ufugaji hufanywa ili kupunguza changamoto zinazokabiliwa na wafugaji
01:0202:46Jamii hujihusisha na mbinu shirikishi za ufugaji.
02:4703:00Chagua eneo la ardhi kwa ajili ya kupanda malisho na uandae ardhi vizuri.
03:1003:19Wakati wa kuandaa ardhi, kata miti midogo ili uweze kulima udongo kwa urahisi.
03:2003:49Lima ardhi, tengeneza mashimo madogo na chimba mifereji ya kutiririsha maji.
03:5004:23Baada ya kupanda mbegu za nyasi, weka maji kwenye mifereji, na palilia baada ya siku 14.
04:2404:33Baada ya siku 21, ongeza maji shambani mara 3 au 4.
04:3404:55Vuna nyasi baada ya siku 45 na uzikaushe kwa siku moja au 2 na kisha uzihifadhi kwa mafungu.
04:5606:00Mbinu za kuhifadhi nyasi husaidia kutoa chakula cha mifugo wakati kinapohitajika.
06:0106:15Kupitia uzalishaji wa nyasi, jamii hukidhi mahitaji yao.
06:1608:48Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *