»Hatua zinazopendekezwa za kilimo mseto cha mahindi na muhogo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=9rzOWvE_jEQ

Muda: 

00:12:38
Imetengenezwa ndani: 
2020

Imetayarishwa na: 

AKILIMO

Muhogo huchukua takribani mwaka mmoja kukomaa na kuvunwa. Kupanda mseto wa zao la muhogo na mazao mengine, kwa mfano mahindi humwezesha mkulima kupata mapato baada ya miezi mitatu.

Muhogo unaweza kulimwa mseto na mazao mengi ambayo ni pamoja na mikunde kama vile maharagwe, soya, mbaazi, karanga, nafaka kama vile mahindi, na mazao mengine ya mizizi kwa mfano viazi vitamu. Kupanda mseto wa mahindi na muhogo hupunguza mavuno ya muhogo, lakini mseto mzuri unahakikisha kuwa unapunguza changamoto hiyo kwa vile mapato yatokanayo na zao la mseto ni makubwa kuliko mapato ya muhogo pekee.

Mambo ya kuzingatia ili kupanda mseto

Ili kupanda mseto wa mahindi na muhogo, chagua aina bora za mihogo na mahindi. Mihogo inapaswa kusimama wima na kutoa matawi ya wastani, huku mahindi yawe aina ya muda mfupi wa ukomaavu kama siku 90.

Weka mbolea kwenye udongo wenye rutuba ya wastani. Ikiwa rutuba ya udongo ni duni sana, weka mbolea ya kikaboni kabla ya kuongeza mbolea ya madini. Viwango vya mbolea vinavyopendekezwa ni gunia sita za 50kg NPK kwa kila hektari wakati wa kupanda. Ongeza mfuko mmoja wa urea ulio na kilo 50 wiki 3 baada ya kupanda. Pia ongeza mfuko mmoja wa kilo 50 za urea wiki 5 baada ya kupanda. Weka mbolea iwapo mapato ya ziada kutokana na ongezeko la mavuno ni makubwa kuliko gharama ya mbolea.

Kupanda, na kuweka mbolea

Ukipanda mihogo kwenye matuta, tenganisha matuta kwa umbali wa 1m. Panda mihogo na mahindi kwa wakati mmoja, huku mashina ya muhogo yakisimishwa au yakiinamishwa. Mahindi hupandwa kwa umbali wa sm 15 kutoka kwa muhogo iwapo matuta yametengenezwa. Iwapo matutu hayajatengenezwa, panda mahindi katikati ya safu za mihogo.

Weka mbolea ya NPK kwenye shimo la kina cha sentimita 5 karibu na mahindi baada ya kupanda 5cm mbali na mahindi. Wiki 3 baada ya kupanda, tengeneza mashimo madogo ya kina kifupi kwa umbali wa sm 20 kutoka kwenye mahindi na uweke mbolea ya urea kwenye mashimo hayo. Kisha weka mfuko mwingine wa urea baada ya wiki 5.

Ikiwa udongo una rutuba sana au unapanga kuweka mbolea, panda mahindi kwenye msongamano mkubwa wa 25cm kati ya mimea, lakini iwapo udongo una rutuba ya wastani, panda kati ya safu kwa umbali wa 50cm.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:40Kupanda mseto wa zao la muhogo na mazao mengine kwa mfano mahindi humwezesha mkulima kupata mapato baada ya miezi 3 au 4.
00:4101:21Unapopanda mahindi na muhogo, haikisha mapato yatokanayo na zao la mseto ni makubwa kuliko mapato ya muhogo pekee.
01:2202:57Ili kupanda mseto, chagua aina bora za mihogo na mahindi.
02:5804:27Weka mbolea kwenye udongo wa rutuba ya wastani.
04:2804:50Weka 50kg NPK kwa kila hektari wakati wa kupanda. Ongeza mfuko mmoja wa urea ulio na kilo 50 wiki 3 baada ya kupanda.
04:5107:34Weka mbolea iwapo mapato ya ziada kutokana na ongezeko la mavuno ni makubwa kuliko gharama ya mbolea
07:3508:46Weka mbolea kulingana na ukubwa la shamba lako.
08:4709:19Weka NPK kwenye shimo la kina cha sentimita 5 , na 5cm mbali na mahindi
09:2009:40Wiki 3 baada ya kupanda, tengeneza mashimo madogo ya kina kifupi kwa umbali wa sm 20 kutoka kwenye mahindi na uweke mbolea ya urea. Rudia utaratibu huu baada ya wiki 5.
09:4110:13Panda mihogo na mahindi kwa wakati mmoja, na umbali wa mita 1 kati yasafu na 80cm ndani ya safui.
10:1410:26Panda mahindi umbali wa sm 15 kutoka kwa muhogo kwa matuta. Panda mahindi katikati ya safu ya mihogo katika eneo tambarare.
10:2710:55Ikiwa udongo una rutuba sana au unapanga kuweka mbolea, panda mahindi kwenye msongamano mkubwa wa 25cm kati ya mimea.
10:5611:16Hakikisha kuna msongamano sahihi wa mimea
11:1712:38Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *