»JINSI YA KUDHIBITI NA KUTIBU UGONJWA WA KIDERI/MDONDO«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=2wt4ctp0Kiw

Muda: 

00:13:42
Imetengenezwa ndani: 
2020

Imetayarishwa na: 

Omas Agro Farm

Ingawa kuku hutoa nyama, mayai, kipato na samadi kwa wafugaji, wana uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa. Ugonjwa wa kideri ndio muuaji mkubwa wa kuku.

Ugonjwa ukishatokea, hakuna tiba na hivyo huua kundi zima la kuku. Ugonjwa huu huathiri ubongo na mfumo wa upumuaji wa kuku, na mara baada ya kuathiriwa, shingo la ndege hujipinda na mabawa hupooza. Ugonjwa huu huenezwa na kuku wagonjwa na watu.

Udhibiti wa ugonjwa wa kideri

Kideri huzuiliwa tu na hutibiwi. Jinsi ya kuzuia kideri ni pamoja na kutenganisha kuku, na kuwachanja. Ufanisi wa chanjo huanza wiki moja baada ya kuchanja ndege. Katika hili, fuata maagizo ya mtengenezaji wa chanjo juu ya jinsi ya kutumia dawa. Unapotumia chanjo, ihifadhi kati ya nyuzijoto 2 hadi 8, na unaposafirisha chanjo shambani,tumia chombo kilicho na barafu ndani ili kudumisha ubaridi.

Vile vile, angalia maagizo yaliyoandikwa kwenye chupa ya chanjo. Kwa matumizi ya chanjo ya La Sota, epuka kuwapa maji kwa kuondoa vyombo vyote vya maji na kuwapa chakula kikavu. Kwa ufyonzaji bora wa chanjo ongeza unga wa maziwa kwenye lita tano za maji. Changanya chanjo kulingana na maagizo yaliyoandikwa kwenye chupa na katika hili, fungulia chupa ya chanjo ndani ya maji.

Gawanya maji yenye dawa katika vyombo tofauti na uviweke kwenye maeneo kadhaa. Chanjo yote iliyochanganywa inapaswa kupewa kwa ndege ndani ya masaa mawili. Hata hivyo, kwa chanjo 1–2 weka tone moja kwenye jicho la kuku, na katika siku za joto chanja ndege asubuhi au kwenye kivuli. Mimina chanjo iliyobaki kwenye choo, osha na kusafisha vyombo baada ya kuchanja. Chanja ndege kila baada ya miezi minne, na pia katika hali ya kuzuia ugonjwa.

Hatimaye, waondoe na uwatenganishe ndege wagonjwa ili wasichanganyike na wenye afya.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:07kuku hutoa nyama, mayai, kipato na samadi kwa wafugaji
00:0800:18Kuku hushambuliwa na magonjwa mbalimbali. Ugonjwa wa kideri ndio muuaji mkubwa wa kuku.
00:1900:38Ugonjwa ukishatokea, hakuna tiba na hivyo huua kundi zima la kuku.
00:3902:01Ugonjwa huu huathiri ubongo na mfumo wa upumuaji wa kuku
02:0202:40Ugonjwa huu huenezwa na kuku wagonjwa na watu.
02:4103:24Kideri huzuiliwa tu na hutibiwi
03:2504:11Kideri hudhibitiwa kwa chanjo.
04:1204:40Ufanisi wa chanjo huanza wiki moja baada ya kuchanja ndege
04:4105:00Fuata maagizo ya mtengenezaji wa chanjo juu ya jinsi ya kutumia dawa.
05:0105:23Hifadhia chanjo kwenye jokofu kati ya nyuzi joto 2 hadi 8 za sentigredi.
05:2406:00Unaposafirisha chanjo shambani,tumia chombo kilicho na barafu ndani
06:0106:05Angalia maagizo yaliyoandikwa kwenye chupa ya chanjo.
06:0606:11Kwa matumizi ya chanjo ya La Sota, usiwape maji kuku.
06:1206:19Chanjo iliyochanganywa inapaswa kutumiwa ndani ya saa 2.
06:2006:25Ondoa vyombo vyote vya maji
06:2606:30Asubuhi, kuku haipaswi kupata maji kwa saa 2.
06:3106:41Wape kuku chakula kikavu
06:4206:54Kwa ufyonzaji bora wa chanjo ongeza unga wa maziwa kwenye lita tano za maji.
06:5507:01Changanya chanjo kulingana na maagizo yaliyoandikwa kwenye chupa
07:0207:23Fungulia chupa ya chanjo ndani ya maji.
07:2407:52Gawanya maji yenye dawa katika vyombo tofauti na uviweke kwenye maeneo kadhaa
07:5308:04Chanjo iliyochanganywa zinapaswa kutolewa kwa ndege ndani ya masaa mawili.
08:0508:028Kwa chanjo 1–2 weka tone moja kwenye jicho la kuku
08:2908:54Katika siku za joto chanja ndege asubuhi
08:5511:03Osha na kusafisha vyombo baada ya kuchanja ndege. Chanja ndege kila baada ya miezi minne.
11:0412:12Dhibiti magonjwa na hakikisha banda la kuku liko safi.
12:1313:05Ondoa na kuwatenganisha ndege wagonjwa ili wasichanganyike na wenye afya.
13:0613:42Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *