»Jinsi ya kurutubisha udongo kwa upanzi wa vitunguu«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/how-make-fertile-soil-onions

Muda: 

00:11:15
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Mazao ya vitunguu yanaweza kuongezeka kwa kupandwa kwenye udongo wenye rutuba, kwa gharama ya chini. Rutuba ya udongo inaweza kuboreshwa kwa kutumia mbolea ya kikaboni au madini.

Vitunguu vinaweza kukuzwa kwenye udongo wa kichanga na udongo wa mfinyanzi kwa kutumia mbolea kama samadi au mbolea oza, kwaani hizi hutoa chakula cha mmea. Mbolea ya kikaboni huchanganywa na udongo angalau kina cha 10cm hadi 20cm ardhini.

Rutuba ya udongo

Nyunyiza maji ya kutosha, kwa sababu maji mengi huzamisha virutubisho chini kwenye udongo. Kufanya udongo kuhifadhi maji zaidi, ongeza mbolea ya kikaboni kabla ya kupandikiza miche ili mimea inawiri. Sambaza mbolea ya kikaboni iliyochanganywa na udongo wa juu, kwaani vitunguu vina mizizi ya kina kifupi.

Weka kwa uangalifu mbolea ya madini kama vile; Nitrojeni, fosforasi na potasiamu wiki 2 baada ya kupandikiza. Nitrojeni husaidia kutengeneza majani, Phosphorus hutengeneza mizizi, na Potasiamu husaidia mimea kustahimili na kuwa sugu dhidi ya magonjwa. Potasiamu inafaa kuongezwa katika udongo wakati wa kupalilia na wakati mmea unaonyesha dalili za upungufu wake.

Tumia mbolea za kemikali au madini kwa kiwango kidogo, kwa kufanya michimbuo midoga sana kati ya mistari ya mimea ili yaweze kufaidika sawa. Epuka kutumia urea miezi 2 kabla ya kuvuna, kwani nitrojeni nyingi hufanya vitunguu kuwa laini. Weka potasiamu au majivu ya kuni ili kuimarisha ngozi ya kitunguu. Mwishowe, weka samadi au mbolea oza ili kulainisha udongo kwaani kuwezesha upenyezaji bora wa maji, na ukuaji bora wa mimea.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:30Vitunguu huhitaji udongo wenye rutuba ili kutoa chakula. vitunguu vina mizizi ya kina kifupi.
01:3101:41Jinsi ya kutunza rutuba ya udongo kwa gharama ndogo.
01:4201:52Mwagilia maji ya kutosha.
01:5303:54Changanya mbolea za kikaboni katika kitalu kabla ya kupandikiza.
03:5504:21Sambaza mbolea ya kikaboni iliyochanganywa na udongo wa juu.
04:2204:33Weka kwa uangalifu mbolea ya madini wiki 2 baada ya kupandikiza.
04:3406:23Ongeza mbolea za madini zilizo na virutubisho vikuu.
06:2406:33Tumia mbolea za kemikali au madini kwa kiwango kidogo.
06:3407:11Fanya michimbuo midoga sana kati ya mistari ya mimea ili uweke mbolea.
07:1207:37Tumia mbolea za majani.
07:3807:49Epuka kutumia urea miezi 2 kabla ya kuvuna.
07:5008:01Weka potasiamu au majivu ya kuni.
08:0209:06Weka samadi au mbolea oza.
09:0711:15Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *