Kuzuia uharibifu baada ya kuvuna: Mnyororo wa thamani wa kilimo

0 / 5. 0

Chanzo:

https://sawbo-animations.org/579

Muda: 

00:06:01
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

SAWBO
Mnyororo wa thamani wa kilimo unajumuisha kila mtu anayefanya kazi ili kupata mazao kutoka kwa mkulima hadi kwa mlaji. Kila mtu aliye katika mnyororo huu ni muhimu.
Mkulima anapotumia mbinu duni za uzalishaji kama vile; kupanda mbegu zisizo bora, kunyunyizia dawa hatari za wadudu, kutopepeta vizuri mahindi wala kuyakausha, na pia kutoyahifadhi vizuri pamoja na kuongeza mawe na taka  kwenye mifuko ili iwe nzito, hupata bei ndogo kutoka kwa mfanyabiashara anapouza mazao yake kutokana na ubora duni wa mazao.

Wafanyabiashara na msagaji

Mfanyabiashara anapouza mahindi kwa msagaji, msagaji pia humpa mfanyabiashara bei ya chini na mfanyabiashara hapati faida yoyote. Msagaji husafisha, hukausha na kusindika mahindi kuwa unga. Mnunuzi hununua unga na kwenda nao nyumbani lakini familia haipendi ladha ya unga huo na kumwacha mtoto mmoja akiwa mgonjwa. Hii hudhuru wanachama wote walio katika mnyororo wa thamani.

Kuongeza thamani

Lakini mkulima anaponunua mbegu bora na kutumia dawa nzuri anapata mavuno mengi na anapokausha mahindi, akayapepeta na kuyahifadhi vizuri na kuamua kuuza na wakulima wengine baada ya kufanya utafiti wa soko kujua taarifa za soko, hupata bei nzuri kutoka kwa mfanyabiashara. Kisha mfanyabiashara huuza mahindi kwa msagaji kwa bei nzuri ambaye husaga mahindi na kuyauzia wanawake wengi kwa bei nzuri, wanawake hupikia familia zao chakula na kila mmoja hupenda chakula hicho. Hapa kila mmoja katika mnyororo wa thamani hufurahia.
Hili linawezekana mbinu nzuri zinapotumika katika uzalishaji, usafirishaji, uhifadhi na usindikaji wa bidhaa, pamoja na wakati wakulima, wafanyabiashara na wasagishaji wanashirikiana kujenga uaminifu na wakati wanapokuwa na taarifa za soko.
Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:42Kila mtu aliye katika mnyororo huu ni muhimu.
00:4302:12Mkulima anapotumia mbinu duni za uzalishaji hupata mavuno duni ambayo husababisha bei ya chini kutoka kwa wafanyabiashara.
02:1303:12Mfanyabiashara anapouza mahindi kwa msagaji, msagaji pia humpa mfanyabiashara bei ya chini na mfanyabiashara hapati faida yoyote.
03:1304:49Mkulima anapotumia mbinu bora za uzalishaji, hupata mavuno mazuri na kila mmoja kwenye mnyororo anapata bei nzuri na mlaji anapata mlo mzuri.
04:5005:30Kila mmoja katika mnyororo hufurahi wakati mbinu bora za uzalishaji zinapotumika, wakati wakulima, wafanyabiashara na wasagaji wanafanya kazi pamoja ili kujenga uaminifu na wakati wametolewa na taarifa za soko.
05:3106:01Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *