»Mbinu bora za kupukuchua, kuchambua, na kukausha mahindi«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/node/10062

Muda: 

00:14:54
Imetengenezwa ndani: 
2018

Imetayarishwa na: 

AFAAS

Baada ya kuvuna mahindi, ni bora kupukuchua, kuchambua, na kukausha mahindi vizuri.

Mahindi yasipo hifadhiwa vizuri baada ya kuvuna, huoza na huharibika kwa haraka. Lakini, yakihifadhiwa kabla hayajakauka vizuri, unyevu unaotoka huleta ukungu, kuvu na mahindi kumea. Nakadhalika, hushambuliwa na wadudu.

Kupukuchua, kuchambua, na kukausha.

Baada ya kutoa maganda, sambaza na uanike mahindi kwa hema/turubai au mahali kavu na safi ili kuyakausha vizuri. Ila , mahindi hayafai kukauka sana , kwasababu yatavunjika wakati wa kupukuchua.

Endelea kwa kutenganisha punje za mahindi na gunzi. kupukuchua mahindi na mbinu za mkono huhitaji mda mrefu japokuwa punje hazivunjiki sana.

Tandaza mahindi kwenye hema, utowe yale yalio vunjika, vumbi na taka kwa kupepeta. Hakikisha kwamba hema unayotumia safi. Kwahivyo, hema lakukaushia lipashe na jua dhidi ya wanyama pia.

Kukausha kunafaa kufanywa kwa saa nne (4) na kufanyika siku ambapo kuna jua kwanzia saa tano asubuhi hadi saa tisa mchana.

Unafaa kugeuza mahindi kila mara wakati unapo yapindua. Ili kukagua kiwango cha ukavu, chota kiasi cha punje kwenye mkono na utikishe usikie kama ina mlio wa kukauka. Ama waweza kuliuma kwa meno punje ili kuhakikisha limekauka. Lakini kabla yakuyahifadhi, unafaa kuacha yapowe kidogo baada ya kuyaanika juani.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:28Mahindi, vuno, kuvuna, Maize,kupukuchua, kuchambua , kukausha na kuhifadhi mahindi ni muhimu kwa kupata hahindi yalio thamani kubwa.
01:2901:50Video hii inaeleza kuhusu kupukuchua, kupepeta, kuchambua na kukausha
01:512:22Mahindi yanafaa kukaushwa vizuri ili kudhiti kuoza na kuharibika kwa haraka.
02:2302:36mahindi hayafai kukauka sana , kwasababu yatavunjika wakati wa kupukuchua.
02:3702:56Kupukuchua ni mchakato wa kutenganisha punje na gunzi
02:5703:23kupukuchua mahindi na chuma huchukuwa mda mfupi kuliko kwa mkono japokuwa punje hazivunjiki sana na mkono.
03:2404:52Unaweza kutumia vidole guba kutoa punje kwa gunzi au kwa kufanya mugusano wa mahindi mawili, nakadhali na zana zingine.
04:5305:39Baada ya kupukuchua, pepeta na pia chambua mahindi
05:4006:23Pepeta mahindi kwa kutumia beseni mbili, hapo mwaga mahindi kutoka kwenye baseni moja kwa ingine mara kadha.
06:2406:42Chambua mahindi kwa kutoa takataka na mahindi yaliovamia.
06:4307:38Kausha mahindi mara tena ili kutoa unyevu.
07:3908:10Unaweza kutumua mwangaza wa jua ili kukausha mahindi
08:1108:40Tandaza mahindi kwenye hema au mahali pa kukaushia safi, geuza mahindi yakianza kukauka.
08:4109:06Kama hauna eno la kukaushia maalum, basi tumia turubai/ hema au jukwaa
09:0709:38Unafaa kugeuza mahindi kila mara wakati unapo yapindua ili yakaueke sawasawa.
09:3910:02Kukausha kunafaa kuchukua mda wa saa tano, na kufanyika siku ambapo kuna jua kwanzia saa tano asubuhi hadi saa tisa mchana.
10:0311:06Hakikisha kwamba safu la punje lilioanikwa halizidi urefu wa nusu kidole
11:0711:22Kiwango cha unyevu kilichopendekezwa ni asilimia kumi nambili
11:2311:55Ili kukagua kiwango cha ukavu, chota kiasi cha punje kwenye mkono na utikishe usikie kama ina mlio wa kukauka. Ama waweza kuliuma kwa meno punje ili kuhakikisha limekauka.
11:5612:33Kabla ya kuhifadhi mahindi, unafaa kuacha yapowe kidogo baada ya kuyakausha.
12:3412:45Chunga mifugo/ wanyama mbali ma mahali.
12:5514:54Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *