»Mchakato wa kuzalisha mbegu za mtama«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=2l5wjFmpdHo

Muda: 

00:07:02
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Coa.Taiwan

Kwa kuwa ni chakula chenye lishe bora, ukuzaji wa mtama umeongezeka kote ulimwenguni. Hata hivyo, uzalishaji wake huathiriwa na mbinu za utunzaji baada ya mavuno ambazo hupunguza ubora na wingi.

Kwa mavuno ya ubora wa juu, mbegu bora ni jambo la kuzingatia. Mtama una uwezo wa kustahimili ukame. Mtama ni zao muhimu kwa ajili ya kutoa malisho na kutengeneza pombe. Kuna haja ya kuratibu muda wa upandaji wa mtama na muda wa kuchanua maua.

Uzalishaji wa mtama

Usimamizi katika kipindi cha ukuaji ni pamoja na; kuondoa magugu, na mbegu zenye kasoro pamoja na kuzuia uharibifu wa ndege ili kufikia viwango vya juu katika ubora na wingi. Hakikisha hakuna aina nyingine za jamii hiyo hiyo katika eneo la uzalishaji wa mbegu na kwa umbali wa mita 300 kutoka ukanda wa kutenganisha, ili kuepuka kuchanganya na zao la kabla ya msimu katika hatua za awali.

Vile vile, fuata taratibu za kawaida za kuondoa mbegu zilizo na kasoro, na magugu kabla ya kuchanua maua. Chukua tahadhari dhidi ya ndege wakati wa kutoa nafaka. kisha fanya vipimo vya unyevu wa mbegu wakati wa kuvuna. Ubora wa mavuno huamuliwa na ukomavu wa mbegu, hali ya hewa, hali ya usafiri, unyevu, uharibifu wa mbegu, ukavu, na halijoto wakati wa kupura. Zingatia hali ya uhifadhi na uwape wakulima mbegu za kutosha kupanda katika msimu ujao. Hifadhi sehemu ya mbegu kwenye ghala kwa ajili ya kupandwa msimu ujao. Weka mtama kwenye vifaa vya kukaushia huku ukiangalia ubora wa mtama.

Chukua vifaa vya kukaushia na uviunganishe na mabomba ya upepo ili kuondoa unyevu wote. Ongeza halijoto na uanze kukausha, huku ukikagua nafaka mara kwa mara wakati wa mchakato wa kukausha. Rekebisha mashine mara moja iwapo imeharibika ili kuzuia kucheleweshwa katika shughuli. Ili kuendelea na mchakato wa kupura, kiwango cha unyevu lazima kipungue kwa 18%. Andaa mahali pa kukaushia mtama, na angalia kama milango ya ghala imefungwa vizuri, na mikanda ya mashine imerekebishwa kwa usahihi.

Pia unafaa kutandaza mbegu sawasawa kwenye ghala iwapo unapura. Chukua sampuli na ufanye vipimo vya kiwango cha unyevu. Kausha nafaka hadi 12% ya unyevu, na uanze mchakato wa kuchagua mbegu. Tandaza safu ya kukaushia mbegu kwa kina kilicho chini ya 40cm. Vipimo vya kiwango cha unyevu lazima vifanywe asubuhi na alasiri.

Anza mchakato wa kuchambua nafaka kwa kurekebisha mashine, na hakikisha vifaa vya kukusanya vumbi viko tayari. Rekebisha mashine za kufungashia na uandae vifurushi au katoni kabla ya kuchambua.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:40Kwa mavuno ya ubora wa juu, mbegu bora ni jambo la kuzingatia
00:4100:50Mtama una uwezo wa kustahimili ukame
00:5100:57Mtama ni zao muhimu kwa ajili ya kutoa malisho na kutengeneza pombe
00:5801:06Ratibu wakati upandaji wa mtama na muda wa kuchanua maua.
01:0701:24Usimamizi ni pamoja na; kuondoa magugu, na mbegu zenye kasoro pamoja na kuzuia uharibifu wa ndege.
01:2501:42Hakikisha hakuna aina nyingine za jamii hiyo hiyo katika eneo la uzalishaji wa mbegu.
01:4301:49Fuata taratibu za kawaida za kuondoa mbegu zilizo na kasoro, na magugu kabla ya maua kuchanua
01:5001:52Chukua tahadhari dhidi ya ndege wakati wa kutoa nafaka
01:5302:01Fanya vipimo vya unyevu wa mbegu wakati wa kuvuna
02:0202:14Ubora wa mavuno huamuliwa na ukomavu wa mbegu, hali ya hewa, hali ya usafiri, unyevu.
02:1502:25Uharibifu wa mbegu, ukavu, na halijoto wakati wa kupura pia huamuliwa na ubora wa mbegu.
02:2602:41Zingatia hali ya uhifadhi na uwape wakulima mbegu za kutosha kupanda katika msimu ujao
02:4202:54Hifadhi sehemu ya mbegu kwa ajili ya kupanda msimu ujao.
02:5503:11Katika ghala, vifaa vya kukaushia lazima vijulikane.
03:1203:31Pakua mtama kwenye vyumba vya kukaushia huku ukiangalia hali ya nafaka. Chukua sampuli ili kupima ubora wa mbegu.
03:3203:44Chukua vifaa vya kukaushia na uviunganishe na mabomba ya upepo ili kuondoa unyevu wote
03:4504:00Ongeza halijoto na uanze kukausha, huku ukikagua nafaka mara kwa mara wakati wa mchakato wa kukausha.
04:0104:06Rekebisha mashine mara moja iwapo imeharibika
04:0704:13Ili kuendelea na mchakato wa kupura, kiwango cha unyevu lazima kipungue
04:1404:19Andaa mahali pa kukaushia mtama
04:2004:27Angalia kama milango ya ghala imefungwa vizuri, na mikanda ya mashine imerekebishwa kwa usahihi.
04:2804:32Iwapo unapura, tandaza mbegu sawasawa kwenye ghala.
04:3304:43Chukua sampuli na ufanye vipimo vya kiwango cha unyevu.
04:4404:52Anze mchakato wa kuchagua mbegu.
04:5304:57Tandaza safu ya kukaushia mbegu kwa kina kilicho chini ya 40cm.
04:5805:07Vipimo vya kiwango cha unyevu lazima vifanywe asubuhi na alasiri.
05:0805:23Anza mchakato wa kuchambua nafaka kwa kurekebisha mashine
05:2405:30Rekebisha mashine za kufungashia na uandae vifurushi kabla ya kuchambua.
05:3107:02Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *