Kwa kuwa ni chakula chenye lishe bora, ukuzaji wa mtama umeongezeka kote ulimwenguni. Hata hivyo, uzalishaji wake huathiriwa na mbinu za utunzaji baada ya mavuno ambazo hupunguza ubora na wingi.
Kwa mavuno ya ubora wa juu, mbegu bora ni jambo la kuzingatia. Mtama una uwezo wa kustahimili ukame. Mtama ni zao muhimu kwa ajili ya kutoa malisho na kutengeneza pombe. Kuna haja ya kuratibu muda wa upandaji wa mtama na muda wa kuchanua maua.
Uzalishaji wa mtama
Usimamizi katika kipindi cha ukuaji ni pamoja na; kuondoa magugu, na mbegu zenye kasoro pamoja na kuzuia uharibifu wa ndege ili kufikia viwango vya juu katika ubora na wingi. Hakikisha hakuna aina nyingine za jamii hiyo hiyo katika eneo la uzalishaji wa mbegu na kwa umbali wa mita 300 kutoka ukanda wa kutenganisha, ili kuepuka kuchanganya na zao la kabla ya msimu katika hatua za awali.
Vile vile, fuata taratibu za kawaida za kuondoa mbegu zilizo na kasoro, na magugu kabla ya kuchanua maua. Chukua tahadhari dhidi ya ndege wakati wa kutoa nafaka. kisha fanya vipimo vya unyevu wa mbegu wakati wa kuvuna. Ubora wa mavuno huamuliwa na ukomavu wa mbegu, hali ya hewa, hali ya usafiri, unyevu, uharibifu wa mbegu, ukavu, na halijoto wakati wa kupura. Zingatia hali ya uhifadhi na uwape wakulima mbegu za kutosha kupanda katika msimu ujao. Hifadhi sehemu ya mbegu kwenye ghala kwa ajili ya kupandwa msimu ujao. Weka mtama kwenye vifaa vya kukaushia huku ukiangalia ubora wa mtama.
Chukua vifaa vya kukaushia na uviunganishe na mabomba ya upepo ili kuondoa unyevu wote. Ongeza halijoto na uanze kukausha, huku ukikagua nafaka mara kwa mara wakati wa mchakato wa kukausha. Rekebisha mashine mara moja iwapo imeharibika ili kuzuia kucheleweshwa katika shughuli. Ili kuendelea na mchakato wa kupura, kiwango cha unyevu lazima kipungue kwa 18%. Andaa mahali pa kukaushia mtama, na angalia kama milango ya ghala imefungwa vizuri, na mikanda ya mashine imerekebishwa kwa usahihi.
Pia unafaa kutandaza mbegu sawasawa kwenye ghala iwapo unapura. Chukua sampuli na ufanye vipimo vya kiwango cha unyevu. Kausha nafaka hadi 12% ya unyevu, na uanze mchakato wa kuchagua mbegu. Tandaza safu ya kukaushia mbegu kwa kina kilicho chini ya 40cm. Vipimo vya kiwango cha unyevu lazima vifanywe asubuhi na alasiri.
Anza mchakato wa kuchambua nafaka kwa kurekebisha mashine, na hakikisha vifaa vya kukusanya vumbi viko tayari. Rekebisha mashine za kufungashia na uandae vifurushi au katoni kabla ya kuchambua.