»Nyigu ambayo hulinda mazao yetu«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/wasp-protects-our-crops

Muda: 

00:08:30
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight, PROINPA

Quinoa ni bidhaa inayohitajika sana, lakini viwavi hufanya upandaji wake kuwa mgumu. Nyigu husaidia kuharibu viwavi na kwa hivyo, kuwezesha kupata mavuno bora.

Wakulima wengi nchini Bolivia wameanza kupanda mashamba makubwa ya quinoa kwa mara ya kwanza, kwa sababu quinoa ni bidhaa maarufu na inayohitajiwa. Lakini tangu mimea ilipoharibiwa, viwavi wanaokula majani na nafaka za quinoa wamegeuka shida kubwa.

Nyigu anayechimba

Baadhi ya nyigu wakubwa huwinda viwavi. Nyigu anayechimba huonekana wakati wa masika na kiangazi. Nyigu huo hula nekta/majimaji ya maua, na maua ya mwituni kama vichaka au nyasi. Viota vyao vina urefu wa 3 cm hadi 7 cm kwenye udongo. Nyigu huwalisha watoto wao viwavi.

Nyigu hudunga kiwavi na kuweka sumu ambayo kumlalisha kiwavi. Kisha, nyugi huleta kiwavi kwenye kiota chake. Katika kiota, nyugi hutaga yai moja kwenye mwili wa kiwavi. Kisha, nyigu hufunga kiota na mchanga ili mdudu mwingine asiingie.

Katika kiota, funza mdogo huanguliwa na kula kiwavi. Kisha funza hujenga kifukofuko na kulala wakati wa majira ya baridi.

Katika wakati wa masika na kiangazi, nyigu zaidi hutoka kwenye vifukofuko vyao na kuanza duru ya maisha tena. Kwaani, nyigu huwinda viwavi kila wakati, na kwa hivyo kulinda mimea ya quinoa, kwa sababu viwavi ndio wadudu amabao huvamia quinoa.

Vidudu vyenye faida.

Badala ya kutumia dawa za kuua wadudu, tunza nyigu na wadudu wengine wazuri. Nyigu huhitaji maua kabla ya kutaga mayai, ili wafyonze umajimaji mtamu (nekta). Kwa hivyo, unafaa kupanda mimea ya asili ili kuwapa chanzo kizuri cha chakula na makao. Na pia, unalinda udongo dhidi ya upepo na mmomomyoko.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:15Wakulima wengi nchini Bolivia wameanza kupanda mashamba makubwa ya quinoa kwa mara ya kwanza, kwa sababu quinoa ni bidhaa maarufu na inayohitajiwa.
01:1601:48Tangu mimea ilipoharibiwa, viwavi wanaokula majani na nafaka za quinoa wamegeuka shida kubwa.
01:4902:46Nyigu anayechimba huonekana wakati wa masika na kiangazi. Nyigu huo hula nekta/majimaji ya maua, na maua ya mwituni kama vichaka au nyasi.
02:4703:25Kwa kupanda mimea ya asili unalinda udongo dhidi ya upepo na mmomomyoko.
03:2603:50Viota vya nyigu vina urefu wa 3 cm hadi 7 cm kwenye udongo.
03:5104:32Nyigu huwalisha watoto wao viwavi.
04:3304:40Nyigu hudunga kiwavi na kuweka majimaji au sumu ambayo kumlalisha kiwavi.
04:4105:09Nyugi huleta kiwavi kwenye kiota chake.
05:1006:28Katika kiota, nyugi hutaga yai moja kwenye mwili wa kiwavi. Kisha, nyigu hufunga kiota na mchanga
06:2906:41Katika kiota, funza mdogo huanguliwa na kula kiwavi. Kisha funza hujenga kifukofuko na kulala wakati wa majira ya baridi.
06:4206:59Katika wakati wa masika na kiangazi, nyigu zaidi hutoka kwenye vifukofuko vyao na kuanza duru ya maisha tena.
07:0007:16Nyigu huhitaji maua kabla ya kutaga mayai, ili wafyonze umajimaji mtamu (nekta).
07:1708:30Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *