»Panda zaidi, ili kuchuma zaidi«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/grow-more-earn-more

Muda: 

00:20:00
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight, CIMMYT, NTV, RWRC

Udongo ukitunzwa au kuhifadhiwa, waweza kupanda mazao ya pili kama mahindi na ngano wakati wa kiangazi. Unaweza kutumia njia mbili: kulima kwa mistari na kupanda kitalu

Udongo hukaa unyevu kwa mda mrefu unapoacha mabaki ya mimea shambani. Lakini wakulima wengi hulima mashamba yao kabla ya kupanda na hawaachi mabaki ya mimea. Kwa hivyo udongo hupoteza rutba na kukauka haraka.

Zao la pili

Wakulima nchini Bangladesh hupenda kutumia mitambo au mashine ambazo hupanda mazao mapema bila kulima shamba lote. Kwa hivyo wanaweza kupanda mazao bora wakati wa kiangazi. Wanavuna zaidi na kuokoa wakati, maji na pesa

Kilimo cha ukanda

kwa aina mbalimbali za mpunga, una uwezo wa kupanda zao la msimu wa kiangazi mapema. Unaweza kuanza kupanda mahindi na ngano wiki moja mapema. Kwa hivyo, haulimi shamba lote baada ya kuvuna mpunga. Trekta ya magurudumu mawili ilio na sanduku maalum inaweza kupanda mbegu na kusambaza mbolea.

Unapoondoa baadhi ya jembe ukalima mstari mwembamba wa ardhi , utaona kwamba mabua hubaki. Udongo uliobaki huendelea kukaa imara na mazao ya pili yanaweza kukua vizuri. visu vinafaa kukata mpunga kwa takribani sentimita 30 juu ya ardhi, ili mabaki wa mimea yatoe unyevu wa udongo kwa muda mrefu.

Kulima ukanda huokoa maji, kazi na mafuta kwa hivyo wakulima na watoa huduma hufaidi.

Kupanda kitalu

Njia nyingine ya kuokoa maji, kazi na pesa ni kupanda kitalu. Kwa hivyo, kuna jembe zinazozunguka ambazo hulima udongo. Udongo huunda maumbo yanayofanana na vitalu.

Ukipanda mimea yako kwenye vitalu ni rahisi kumwagilia, kuokoa maji, na kudhibiti panya. Vitalu husababisha upenyezi wa mwangaza wa jua kupitia, ambayo panya hawapendi, na kumwagilia hufanya udongo kuwa thabiti kwenye mifereji, kwa hivyo panya hukaa huko chini.

Mashine ya upandaji wa kitalu husambaza mbolea, pamoja na kupanda mbegu, kama vile trekta ya kulima.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0002:48Wakulima nchini Bangladesh hupata mavuno bora katika mazao ya pili
02:4903:09Udongo hukaa unyevu kwa mda mrefu unapoacha mabaki ya mimea shambani
03:1005:22Wakulima wengi hulima mashamba yao kabla ya kupanda na hawaachi mabaki ya mimea.
05:2306:11Ukipanda mazao mapema unaweza kuvuna zaidi na kuokoa wakati, maji na pesa
06:1209:05Trekta ya magurudumu mawili ilio na sanduku maalum inaweza kupanda mbegu pamoja na kusambaza mbolea.
09:0611:38Kwa kilimo cha ukanda , haulimi shamba lote baada ya kuvuna mpunga.
11:3912:15Visu vinafaa kukata mpunga kwa takribani sentimita 30 juu ya ardhi, ili mabaki wa mimea yatoe unyevu wa udongo kwa muda mrefu.
12:1613:08Njia nyingine ya kuokoa maji, kazi na pesa ni kupanda kitalu
13:0914:43Ukipanda mimea yako kwenye vitalu ni rahisi kumwagilia, kuokoa maji, na kudhibiti panya
14:4416:20Ukipanda mimea yako kwenye vitalu ni rahisi kumwagilia, kuokoa maji, na kudhibiti panya
16:2117:44Sanduku maalum za mbegu zina jembe zinazozunguka ambazo hulima udongo.
17:4520:00Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *