Hatua za kupanda vitunguu saumu

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=tBD-c8xS4Hk&t=151s

Muda: 

00:04:28
Imetengenezwa ndani: 
2022

Imetayarishwa na: 

Business Ideas English
Kilimo cha vitunguu saumu kinahitaji kazi kidogo na gharama kidogo, lakini kina wateja wengi na faida kubwa. Vitunguu hustawi vyema katika hali mbalimbali za hewa.
Kitunguu saumu hupandwa kwa mbegu na huvunwa kati ya siku 135-150 baada ya kupandwa. Kawaida majani ya kitunguu saumu yanapoanza kuwa ya manjano hii ni dalili kwamba mmea kitunguu kiko tayari kuvunwa. Kwa kawaida kitunguu saumu hupendelea halijoto ya wastani, udongo tifutifu, udongo wa kichanga au udongo wa mfinyanzi kwa ukuaji bora.

Kupanda

Wakati wa kupanda kitunguu saumu tumia kilo 150- 200 za mbegu zenye afya ili kupanda hekta 1, na panda kwa mitaro au matuta. Panda mbegu za vitunguu kwenye kina cha sentimita 5.5-7.5 huku ncha za mbegu zikitazama juu.  Muachano kati ya mimea ni 15cm, na mbegu hufunikwa na udongo laini. Panda ama  katika msimu wa Juni-Julai au Oktoba-Novemba katika matuta ya 15cm, na lazima mimea imwagiliwe maji kidogo.

Mbolea na umwagiliaji

Kwanza, ongeza tani 20 ya samadi ya kikaboni iliyooza vizuri kwa hekta ili kuongeza kiwango cha rutuba ya udongo. Baada ya hapo, ongeza mbolea ya NPK kwa kiwango cha kilo 60 kwa hekta, na siku 30 baada ya kupanda weka 10kg ya borax kwa hekta ili kuongeza ukubwa wa vitunguu. Hakikisha unamwagilia shamba mara baada ya kupanda, na dhibiti magugu kwa kutumia mikono. Pia, chunguza wadudu na magonjwa, na baada ya kuvuna kuweka vitunguu chini ya kivuli kwa siku 2-3. Mwishowe, ondoa mabua yaliyokauka, safi vitunguu, vichambue na viainishe.
Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:18Kilimo cha vitunguu saumu kinahitaji kazi kidogo na gharama kidogo, lakini kina wateja wengi na faida kubwa
00:1900:47Vitunguu vinaweza kutumika kama dawa na kama kiungo cha chakula.
00:4801:08Vitunguu saumu hustawi katika hali mbalimbali za hewa na hupendelea halijoto ya wastani.
01:0901:19Kwa kawaida kitunguu saumu hupendelea halijoto ya wastani, udongo tifutifu, udongo wa kichanga au udongo wa mfinyanzi kwa ukuaji bora.
01:2001:46Kitunguu saumu hupandwa kwa mbegu na huvunwa kati ya siku 135-150 baada ya kupandwa
01:4702:09Panda mbegu za vitunguu kwenye kina cha sentimita 5.5-7.5 huku ncha za mbegu zikitazama juu
02:1002:32Panda ama katika msimu wa Juni-Julai au Oktoba-Novemba katika matuta ya 15cm
02:3302:55ongeza tani 20 ya samadi ya kikaboni iliyooza vizuri kwa hekta ili kuongeza kiwango cha rutuba ya udongo.
02:5603:23siku 30 baada ya kupanda weka 10kg ya borax kwa hekta ili kuongeza ukubwa wa vitunguu
03:2404:07Hakikisha unamwagilia shamba mara baada ya kupanda, na dhibiti magugu kwa kutumia mikono.
04:0804:28Pia, chunguza wadudu na magonjwa, na baada ya kuvuna kuweka vitunguu chini ya kivuli kwa siku 2-3.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *